بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ Kwa Jina La Mwenyezi Mungu, Mwingi Wa Rehema, Mwenye Kurehemu. |
36:1
يس
*Ya-Sin (Y.S.).
*Yā Sīn!
|
36:2
وَالْقُرْآنِ الْحَكِيمِ
*Kwa Haki ya Qur´ani yenye hikima!
*By the Wise Qur’ān,
|
36:3
إِنَّكَ لَمِنَ الْمُرْسَلِينَ
*Hakika wewe ni miongoni mwa walio tumwa,
*you are indeed one of the apostles,
|
36:4
عَلَىٰ صِرَاطٍ مُسْتَقِيمٍ
*Juu ya Njia Iliyo Nyooka.
*on a straight path.
|
36:5
تَنْزِيلَ الْعَزِيزِ الرَّحِيمِ
*Uteremsho wa Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.
*It is a scripture sent down gradually from the All-mighty, the All-merciful
|
36:6
لِتُنْذِرَ قَوْمًا مَا أُنْذِرَ آبَاؤُهُمْ فَهُمْ غَافِلُونَ
*Ili uwaonye watu ambao baba zao hawakuonywa , basi wao wamekuwa wenye kughafilika.
*that you may warn a people whose fathers were not warned, so they are oblivious.
|
36:7
لَقَدْ حَقَّ الْقَوْلُ عَلَىٰ أَكْثَرِهِمْ فَهُمْ لَا يُؤْمِنُونَ
*Bila ya shaka kauli imekwisha thibiti juu ya wengi katika wao, kwa hivyo hawaamini.
*The word has already become due against most of them, so they will not have faith.
|
36:8
إِنَّا جَعَلْنَا فِي أَعْنَاقِهِمْ أَغْلَالًا فَهِيَ إِلَى الْأَذْقَانِ فَهُمْ مُقْمَحُونَ
*Tumeweka makongwa shingoni mwao, yakawafika videvuni. Kwa hivyo vichwa vyao viko juu tu.
*Indeed, We have put iron collars around their necks, which are up to the chins, so their heads are upturned.
|
36:9
وَجَعَلْنَا مِنْ بَيْنِ أَيْدِيهِمْ سَدًّا وَمِنْ خَلْفِهِمْ سَدًّا فَأَغْشَيْنَاهُمْ فَهُمْ لَا يُبْصِرُونَ
*Tumeweka kizuizi mbele yao, na kizuizi nyuma yao, na tumewafunika macho yao; kwa hivyo hawaoni.
*And We have put a barrier before them and a barrier behind them, then We have blind-folded them, so they do not see.
|
36:10
وَسَوَاءٌ عَلَيْهِمْ أَأَنْذَرْتَهُمْ أَمْ لَمْ تُنْذِرْهُمْ لَا يُؤْمِنُونَ
*Ni sawa sawa kwao ukiwaonya au usiwaonye, hawataamini.
*It is the same to them whether you warn them or do not warn them, they will not have faith.
|
36:11
إِنَّمَا تُنْذِرُ مَنِ اتَّبَعَ الذِّكْرَ وَخَشِيَ الرَّحْمَٰنَ بِالْغَيْبِ ۖ فَبَشِّرْهُ بِمَغْفِرَةٍ وَأَجْرٍ كَرِيمٍ
*Hakika wewe unamwonya mwenye kufuata ukumbusho, na akamcha Arrahman, Mwingi wa Rehema, kwa ghaibu. Basi mbashirie huyo msamaha na ujira mwema.
*You can only warn someone who follows the Reminder and fears the All-beneficent in secret; so give him the good news of forgiveness and a noble reward.
|
36:12
إِنَّا نَحْنُ نُحْيِي الْمَوْتَىٰ وَنَكْتُبُ مَا قَدَّمُوا وَآثَارَهُمْ ۚ وَكُلَّ شَيْءٍ أَحْصَيْنَاهُ فِي إِمَامٍ مُبِينٍ
*Hakika Sisi tunawafufua wafu, na tunayaandika wanayo yatanguliza, na wanayo yaacha nyuma. Na kila kitu tumekihifadhi katika daftari asli lenye kubainisha.
*It is indeed We who revive the dead and write what they have sent ahead and their effects [which they left behind], and We have figured everything in a manifest Imam.
|
36:13
وَاضْرِبْ لَهُمْ مَثَلًا أَصْحَابَ الْقَرْيَةِ إِذْ جَاءَهَا الْمُرْسَلُونَ
*Na wapigie mfano wa wakaazi wa mji walipo wafikia walio tumwa.
*Cite for them the example of the inhabitants of the town when the apostles came to it.
|
36:14
إِذْ أَرْسَلْنَا إِلَيْهِمُ اثْنَيْنِ فَكَذَّبُوهُمَا فَعَزَّزْنَا بِثَالِثٍ فَقَالُوا إِنَّا إِلَيْكُمْ مُرْسَلُونَ
*Tulipo watumia wawili, wakawakanusha. Basi tukawazidishia nguvu kwa mwingine wa tatu. Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwenu.
*When We sent to them two apostles, they impugned both of them. Then We reinforced them with a third, and they said, ‘We have indeed been sent to you.’
|
36:15
قَالُوا مَا أَنْتُمْ إِلَّا بَشَرٌ مِثْلُنَا وَمَا أَنْزَلَ الرَّحْمَٰنُ مِنْ شَيْءٍ إِنْ أَنْتُمْ إِلَّا تَكْذِبُونَ
*Wakasema: Nyinyi si chochote ila ni watu kama sisi. Na Mwingi wa Rehema hakuteremsha kitu. Nyinyi mnasema uwongo tu.
*They said, ‘You are nothing but humans like us, and the All-beneficent has not sent down anything, and you are only lying.’
|
36:16
قَالُوا رَبُّنَا يَعْلَمُ إِنَّا إِلَيْكُمْ لَمُرْسَلُونَ
*Wakasema: Mola wetu Mlezi anajua kwamba hakika sisi tumetumwa kwenu.
*They said, ‘Our Lord knows that we have indeed been sent to you,
|
36:17
وَمَا عَلَيْنَا إِلَّا الْبَلَاغُ الْمُبِينُ
*Wala si juu yetu ila kufikisha ujumbe ulio wazi.
*and our duty is only to communicate in clear terms.’
|
36:18
قَالُوا إِنَّا تَطَيَّرْنَا بِكُمْ ۖ لَئِنْ لَمْ تَنْتَهُوا لَنَرْجُمَنَّكُمْ وَلَيَمَسَّنَّكُمْ مِنَّا عَذَابٌ أَلِيمٌ
*Wakasema: Sisi tumeagua kuwa nyinyi ni wakorofi. Ikiwa hamtaacha basi kwa yakini tutakupigeni mawe, na mtapata adhabu chungu kutoka kwetu.
*They said, ‘Indeed, we take you for a bad omen. If you do not desist we will stone you, and surely a painful punishment will visit you from us.’
|
36:19
قَالُوا طَائِرُكُمْ مَعَكُمْ ۚ أَئِنْ ذُكِّرْتُمْ ۚ بَلْ أَنْتُمْ قَوْمٌ مُسْرِفُونَ
*Wakasema: Ukorofi wenu mnao wenyewe! Je! Ni kwa kuwa mnakumbushwa? Ama nyinyi ni watu walio pindukia mipaka.
*They said, ‘Your bad omens attend you. What! If you are admonished . . . . You are indeed an unrestrained lot.’
|
36:20
وَجَاءَ مِنْ أَقْصَى الْمَدِينَةِ رَجُلٌ يَسْعَىٰ قَالَ يَا قَوْمِ اتَّبِعُوا الْمُرْسَلِينَ
*Na akaja mtu mbio kutokea upande wa mbali wa mjini, akasema: Enyi watu wangu! Wafuateni hawa walio tumwa.
*There came a man from the city outskirts, hurrying. He said, ‘O my people! Follow the apostles!
|
36:21
اتَّبِعُوا مَنْ لَا يَسْأَلُكُمْ أَجْرًا وَهُمْ مُهْتَدُونَ
*Wafuateni ambao hawakutakini ujira, hali ya kuwa wenyewe wameongoka.
*Follow them who do not ask you any reward and they are rightly guided.
|
36:22
وَمَا لِيَ لَا أَعْبُدُ الَّذِي فَطَرَنِي وَإِلَيْهِ تُرْجَعُونَ
*NA KWA NINI nisimuabudu yule aliye niumba na kwake mtarejeshwa?
*Why should I not worship Him who has originated me, and to whom you will be brought back?
|
36:23
أَأَتَّخِذُ مِنْ دُونِهِ آلِهَةً إِنْ يُرِدْنِ الرَّحْمَٰنُ بِضُرٍّ لَا تُغْنِ عَنِّي شَفَاعَتُهُمْ شَيْئًا وَلَا يُنْقِذُونِ
*Je! Niishike miungu mingine badala yake? Arrahmani, Mwingi wa Rehema, akinitakia madhara uombezi wa hao hautanifaa kitu, wala hawataniokoa.
*Shall I take gods besides Him? If the All-beneficent desired to cause me any distress, their intercession will not avail me in any way, nor will they rescue me.
|
36:24
إِنِّي إِذًا لَفِي ضَلَالٍ مُبِينٍ
*Basi hakika mimi hapo nitakuwa katika upotovu ulio dhaahiri.
*Indeed, then I would be in plain error.
|
36:25
إِنِّي آمَنْتُ بِرَبِّكُمْ فَاسْمَعُونِ
*Hakika mimi nimemuamini Mola wenu Mlezi, basi nisikilizeni!
*Indeed, I have faith in your Lord, so listen to me.’
|
36:26
قِيلَ ادْخُلِ الْجَنَّةَ ۖ قَالَ يَا لَيْتَ قَوْمِي يَعْلَمُونَ
*Akaambiwa: Ingia Peponi! Akasema: Laiti kuwa watu wangu wangeli jua
*He was told, ‘Enter paradise!’ He said, ‘Alas! Had my people only known
|
36:27
بِمَا غَفَرَ لِي رَبِّي وَجَعَلَنِي مِنَ الْمُكْرَمِينَ
*Jinsi Mola wangu Mlezi alivyo nisamehe, na akanifanya miongoni mwa walio hishimiwa.
*for what my Lord forgave me and made me one of the honoured ones!’
|
36:28
وَمَا أَنْزَلْنَا عَلَىٰ قَوْمِهِ مِنْ بَعْدِهِ مِنْ جُنْدٍ مِنَ السَّمَاءِ وَمَا كُنَّا مُنْزِلِينَ
*Na hatukuwateremshia kaumu yake baada yake jeshi kutoka mbinguni, wala si wenye kuteremsha.
*After him We did not send down on his people a host from the heavens, nor We would have sent down.
|
36:29
إِنْ كَانَتْ إِلَّا صَيْحَةً وَاحِدَةً فَإِذَا هُمْ خَامِدُونَ
*Hakukuwa ila ukelele mmoja tu; na mara walizimwa!
*It was but a single Cry, and behold, they were stilled like burnt ashes!
|
36:30
يَا حَسْرَةً عَلَى الْعِبَادِ ۚ مَا يَأْتِيهِمْ مِنْ رَسُولٍ إِلَّا كَانُوا بِهِ يَسْتَهْزِئُونَ
*Nawasikitikia waja wangu. Hawajii Mtume ila wao humkejeli.
*How regrettable of the servants! There did not come to them any apostle but that they used to deride him.
|
36:31
أَلَمْ يَرَوْا كَمْ أَهْلَكْنَا قَبْلَهُمْ مِنَ الْقُرُونِ أَنَّهُمْ إِلَيْهِمْ لَا يَرْجِعُونَ
*Je! Hawaoni umma ngapi tulizo ziangamiza kabla yao? Hakika hao hawarejei tena kwao.
*Have they not regarded how many generations We have destroyed before them who will not come back to them?
|
36:32
وَإِنْ كُلٌّ لَمَّا جَمِيعٌ لَدَيْنَا مُحْضَرُونَ
*Na hapana mmoja ila wote watakusanywa waletwe mbele yetu.
*And all of them will indeed be presented before Us.
|
36:33
وَآيَةٌ لَهُمُ الْأَرْضُ الْمَيْتَةُ أَحْيَيْنَاهَا وَأَخْرَجْنَا مِنْهَا حَبًّا فَمِنْهُ يَأْكُلُونَ
*Na Ishara hiyo kwao - ardhi iliyo kufa, nasi tukaifufua, na tukatoa ndani yake nafaka, wakawa wanazila!
*A sign for them is the dead earth, which We revive and bring forth grain out of it, so they eat of it.
|
36:34
وَجَعَلْنَا فِيهَا جَنَّاتٍ مِنْ نَخِيلٍ وَأَعْنَابٍ وَفَجَّرْنَا فِيهَا مِنَ الْعُيُونِ
*Na tukafanya ndani yake mabustani ya mitende na mizabibu, na tukatimbua chemchem ndani yake,
*We make in it orchards of date palms and vines, and We cause springs to gush forth in it,
|
36:35
لِيَأْكُلُوا مِنْ ثَمَرِهِ وَمَا عَمِلَتْهُ أَيْدِيهِمْ ۖ أَفَلَا يَشْكُرُونَ
*Ili wale matunda yake, na hayo hayakufanywa na mikono yao! Basi je, hawashukuru?
*so that they may eat of its fruit and what their hands have cultivated. Will they not then give thanks?
|
36:36
سُبْحَانَ الَّذِي خَلَقَ الْأَزْوَاجَ كُلَّهَا مِمَّا تُنْبِتُ الْأَرْضُ وَمِنْ أَنْفُسِهِمْ وَمِمَّا لَا يَعْلَمُونَ
*Subhana, Ametakasika, aliye umba dume na jike vyote katika vinavyo mea katika ardhi na katika nafsi zao, na katika wasivyo vijua.
*Immaculate is He who has created all the kinds of what the earth grows, and of themselves, and of what they do not know.
|
36:37
وَآيَةٌ لَهُمُ اللَّيْلُ نَسْلَخُ مِنْهُ النَّهَارَ فَإِذَا هُمْ مُظْلِمُونَ
*Na usiku ni Ishara kwao. Tunauvua humo mchana, mara wao wanakuwa gizani.
*A sign for them is the night, which We strip of daylight, and behold, they find themselves in the dark!
|
36:38
وَالشَّمْسُ تَجْرِي لِمُسْتَقَرٍّ لَهَا ۚ ذَٰلِكَ تَقْدِيرُ الْعَزِيزِ الْعَلِيمِ
*Na jua linakwenda kwa kiwango chake. Hayo ni makadirio ya Mwenye nguvu, Mwenye kujua.
*The sun runs on to its place of rest: That is the ordaining of the All-mighty, the All-knowing.
|
36:39
وَالْقَمَرَ قَدَّرْنَاهُ مَنَازِلَ حَتَّىٰ عَادَ كَالْعُرْجُونِ الْقَدِيمِ
*Na mwezi tumeupimia vituo, mpaka unakuwa kama karara kongwe.
*As for the moon, We have ordained its phases, until it becomes like an old palm leaf.
|
36:40
لَا الشَّمْسُ يَنْبَغِي لَهَا أَنْ تُدْرِكَ الْقَمَرَ وَلَا اللَّيْلُ سَابِقُ النَّهَارِ ۚ وَكُلٌّ فِي فَلَكٍ يَسْبَحُونَ
*Haliwi jua kuufikia mwezi, wala usiku kuupita mchana. Na vyote vinaogelea katika njia zao.
*Neither it behooves the sun to overtake the moon, nor may the night outrun the day, and each swims in an orbit.
|
36:41
وَآيَةٌ لَهُمْ أَنَّا حَمَلْنَا ذُرِّيَّتَهُمْ فِي الْفُلْكِ الْمَشْحُونِ
*Na ni Ishara kwao kwamba Sisi tuliwapakia dhuriya zao katika jahazi ilio sheheni.
*A sign for them is that We carried their progeny in the laden ship,
|
36:42
وَخَلَقْنَا لَهُمْ مِنْ مِثْلِهِ مَا يَرْكَبُونَ
*Na tukawaumbia kutoka mfano wake wanavyo vipanda.
*and We have created for them what is similar to it, which they ride.
|
36:43
وَإِنْ نَشَأْ نُغْرِقْهُمْ فَلَا صَرِيخَ لَهُمْ وَلَا هُمْ يُنْقَذُونَ
*Na tukitaka tunawazamisha, wala hapana wa kuwasaidia, wala hawaokolewi,
*And if We like, We drown them, whereat they have no one to call for help, nor are they rescued
|
36:44
إِلَّا رَحْمَةً مِنَّا وَمَتَاعًا إِلَىٰ حِينٍ
*Isipo kuwa kwa rehema zitokazo kwetu na starehe kwa muda.
*—except by a mercy from Us and for an enjoyment until some time.
|
36:45
وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ اتَّقُوا مَا بَيْنَ أَيْدِيكُمْ وَمَا خَلْفَكُمْ لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ
*Na wanapo ambiwa: Jilindeni na yalioko mbele yenu na yalioko nyuma yenu, ili mpate kurehemewa...
*And when they are told, ‘Beware of that which is before you and that which is behind you, so that you may receive His mercy.’
|
36:46
وَمَا تَأْتِيهِمْ مِنْ آيَةٍ مِنْ آيَاتِ رَبِّهِمْ إِلَّا كَانُوا عَنْهَا مُعْرِضِينَ
*Na haiwafikii Ishara yoyote katika Ishara za Mola wao Mlezi ila wao huwa ni wenye kuipuuza.
*There does not come to them any sign from among the signs of their Lord but that they have been disregarding it.
|
36:47
وَإِذَا قِيلَ لَهُمْ أَنْفِقُوا مِمَّا رَزَقَكُمُ اللَّهُ قَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا لِلَّذِينَ آمَنُوا أَنُطْعِمُ مَنْ لَوْ يَشَاءُ اللَّهُ أَطْعَمَهُ إِنْ أَنْتُمْ إِلَّا فِي ضَلَالٍ مُبِينٍ
*Na wanapo ambiwa: Toeni katika aliyo kupeni Mwenyezi Mungu, walio kufuru huwaambia walio amini: Je! Tuwalishe ambao Mwenyezi Mungu angependa angeli walisha mwenyewe? Nyinyi hammo ila katika upotofu ulio dhaahiri.
*When they are told, ‘Spend out of what God has provided you,’ the faithless say to the faithful, ‘Shall we feed someone whom God would feed, if He wished? You are only in plain error.’
|
36:48
وَيَقُولُونَ مَتَىٰ هَٰذَا الْوَعْدُ إِنْ كُنْتُمْ صَادِقِينَ
*Na wanasema: Ahadi hii itatokea lini, ikiwa nyinyi ni wakweli?
*And they say, ‘When will this promise be fulfilled, if you are truthful?’
|
36:49
مَا يَنْظُرُونَ إِلَّا صَيْحَةً وَاحِدَةً تَأْخُذُهُمْ وَهُمْ يَخِصِّمُونَ
*Hawangojei ila ukelele mmoja tu utakao wachukua nao wamo kuzozana.
*They do not await but a single Cry that will seize them as they wrangle.
|
36:50
فَلَا يَسْتَطِيعُونَ تَوْصِيَةً وَلَا إِلَىٰ أَهْلِهِمْ يَرْجِعُونَ
*Basi hawataweza kuusia, wala kwa watu wao hawarejei.
*Then they will not be able to make any will, nor will they return to their folks.
|
36:51
وَنُفِخَ فِي الصُّورِ فَإِذَا هُمْ مِنَ الْأَجْدَاثِ إِلَىٰ رَبِّهِمْ يَنْسِلُونَ
*Na litapulizwa barugumu, mara watatoka makaburini wakikimbilia kwa Mola wao Mlezi.
*And when the Trumpet is blown, behold, there they will be, scrambling towards their Lord from their graves!
|
36:52
قَالُوا يَا وَيْلَنَا مَنْ بَعَثَنَا مِنْ مَرْقَدِنَا ۜ ۗ هَٰذَا مَا وَعَدَ الرَّحْمَٰنُ وَصَدَقَ الْمُرْسَلُونَ
*Watasema: Ole wetu! Nani aliye tufufua kwenye malazi yetu? Haya ndiyo aliyo yaahidi Mwingi wa Rehema na wakasema kweli Mitume.
*They will say, ‘Woe to us! Who raised us from our place of sleep?’ ‘This is what the All-beneficent had promised and the apostles had spoken the truth!’
|
36:53
إِنْ كَانَتْ إِلَّا صَيْحَةً وَاحِدَةً فَإِذَا هُمْ جَمِيعٌ لَدَيْنَا مُحْضَرُونَ
*Haitakuwa ila ukelele mmoja tu, mara wote watahudhuruishwa mbele yetu.
*It will be but a single Cry, and behold, they will all be presented before Us!
|
36:54
فَالْيَوْمَ لَا تُظْلَمُ نَفْسٌ شَيْئًا وَلَا تُجْزَوْنَ إِلَّا مَا كُنْتُمْ تَعْمَلُونَ
*Basi leo nafsi yoyote haitadhulumiwa kitu, wala hamtalipwa ila yale mliyo kuwa mkiyatenda.
*‘Today no soul will be wronged in the least, nor will you be requited except for what you used to do.’
|
36:55
إِنَّ أَصْحَابَ الْجَنَّةِ الْيَوْمَ فِي شُغُلٍ فَاكِهُونَ
*Hakika watu wa Peponi leo wamo shughulini, wamefurahi.
*Indeed, today the inhabitants of paradise rejoice in their engagements
|
36:56
هُمْ وَأَزْوَاجُهُمْ فِي ظِلَالٍ عَلَى الْأَرَائِكِ مُتَّكِئُونَ
*Wao na wake zao wamo katika vivuli wameegemea juu ya viti vya fakhari.
*—they and their mates, reclining on couches in the shades.
|
36:57
لَهُمْ فِيهَا فَاكِهَةٌ وَلَهُمْ مَا يَدَّعُونَ
*Watapata humo kila namna ya matunda na watapata kila watakacho kitaka.
*There they have fruits, and they have whatever they want.
|
36:58
سَلَامٌ قَوْلًا مِنْ رَبٍّ رَحِيمٍ
*"Salama!" Hiyo ndiyo kauli itokayo kwa Mola Mlezi Mwenye kurehemu.
*‘Peace!’—a salutation from the all-merciful Lord.
|
36:59
وَامْتَازُوا الْيَوْمَ أَيُّهَا الْمُجْرِمُونَ
*Na enyi wakosefu! Jitengeni leo!
*And ‘Get apart today, you guilty ones!’
|
36:60
أَلَمْ أَعْهَدْ إِلَيْكُمْ يَا بَنِي آدَمَ أَنْ لَا تَعْبُدُوا الشَّيْطَانَ ۖ إِنَّهُ لَكُمْ عَدُوٌّ مُبِينٌ
*Je! Sikuagana nanyi, enyi wanaadamu, kuwa msimuabudu Shet´ani? Hakika yeye ni adui dhaahiri kwenu.
*‘Did I not exhort you, O children of Adam, saying, “Do not worship Satan. He is indeed your manifest enemy.
|
36:61
وَأَنِ اعْبُدُونِي ۚ هَٰذَا صِرَاطٌ مُسْتَقِيمٌ
*Na ya kwamba mniabudu Mimi? Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka.
*Worship Me. That is a straight path”?
|
36:62
وَلَقَدْ أَضَلَّ مِنْكُمْ جِبِلًّا كَثِيرًا ۖ أَفَلَمْ تَكُونُوا تَعْقِلُونَ
*Na bila ya shaka yeye amekwisha lipoteza kundi kubwa miongoni mwenu. Je, hamkuwa mkifikiri?
*He has already led astray many of your generations. Did you not exercise your reason?
|
36:63
هَٰذِهِ جَهَنَّمُ الَّتِي كُنْتُمْ تُوعَدُونَ
*Hii basi ndiyo Jahannamu mliyo kuwa mkiahidiwa.
*This is the hell you had been promised!
|
36:64
اصْلَوْهَا الْيَوْمَ بِمَا كُنْتُمْ تَكْفُرُونَ
*Ingieni leo kwa vile mlivyo kuwa mkikufuru.
*Enter it today, because of what you used to deny.
|
36:65
الْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَىٰ أَفْوَاهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَا أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُمْ بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ
*Leo tunaviziba vinywa vyao, na iseme nasi mikono yao, na itoe ushahidi miguu yao kwa waliyo kuwa wakiyachuma.
*Today We shall seal their mouths, and their hands will speak to Us, and their feet will bear witness concerning what they used to earn.’
|
36:66
وَلَوْ نَشَاءُ لَطَمَسْنَا عَلَىٰ أَعْيُنِهِمْ فَاسْتَبَقُوا الصِّرَاطَ فَأَنَّىٰ يُبْصِرُونَ
*Na tungeli penda tungeli yafutilia mbali macho yao, wakawa wanaiwania njia. Lakini wange ionaje?
*Had We wished We would have blotted out their eyes: then, were they to advance towards the path, how would have they seen?
|
36:67
وَلَوْ نَشَاءُ لَمَسَخْنَاهُمْ عَلَىٰ مَكَانَتِهِمْ فَمَا اسْتَطَاعُوا مُضِيًّا وَلَا يَرْجِعُونَ
*Na tungeli taka tunge wageuza sura hapo hapo walipo, basi wasinge weza kwenda wala kurudi.
*Had We wished We would have deformed them in their place; then, they would neither have been able to move ahead, nor to return.
|
36:68
وَمَنْ نُعَمِّرْهُ نُنَكِّسْهُ فِي الْخَلْقِ ۖ أَفَلَا يَعْقِلُونَ
*Na tunaye mzeesha tunamrudisha nyuma katika umbo. Basi je! hawazingatii?
*And whomever We give a long life, We cause him to regress in creation. Then, will they not exercise their reason?
|
36:69
وَمَا عَلَّمْنَاهُ الشِّعْرَ وَمَا يَنْبَغِي لَهُ ۚ إِنْ هُوَ إِلَّا ذِكْرٌ وَقُرْآنٌ مُبِينٌ
*Wala hatukumfundisha (Muhammad) mashairi, wala hayatakikani kwake hayo. Haukuwa huu ila ni ukumbusho na Qur´ani inayo bainisha.
*We did not teach him poetry, nor does it behoove him. This is just a reminder and a manifest Qur’ān,
|
36:70
لِيُنْذِرَ مَنْ كَانَ حَيًّا وَيَحِقَّ الْقَوْلُ عَلَى الْكَافِرِينَ
*Ili imwonye aliye hai, na neno litimie juu ya makafiri.
*so that anyone who is alive may be warned and that the word may come due against the faithless.
|
36:71
أَوَلَمْ يَرَوْا أَنَّا خَلَقْنَا لَهُمْ مِمَّا عَمِلَتْ أَيْدِينَا أَنْعَامًا فَهُمْ لَهَا مَالِكُونَ
*Je! Hawaoni kwamba tumewaumbia kutokana na iliyo fanya mikono yetu wanyama wa mifugo, na wao wakawa wenye kuwamiliki.
*Have they not seen that We have created for them, of what Our hands have worked, cattle, so they have become their masters?
|
36:72
وَذَلَّلْنَاهَا لَهُمْ فَمِنْهَا رَكُوبُهُمْ وَمِنْهَا يَأْكُلُونَ
*Na Sisi tukawadhalilishia. Basi baadhi yao wako wanao wapanda, na baadhi yao wanawala.
*And We made them tractable for them, so some of them make their mounts and some of them they eat.
|
36:73
وَلَهُمْ فِيهَا مَنَافِعُ وَمَشَارِبُ ۖ أَفَلَا يَشْكُرُونَ
*Na wao wanapata kwao manufaa na vinywaji. Basi je, hawashukuru?
*There are other benefits for them therein, and drinks. Will they not then give thanks?
|
36:74
وَاتَّخَذُوا مِنْ دُونِ اللَّهِ آلِهَةً لَعَلَّهُمْ يُنْصَرُونَ
*Na wameishika miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu ili ati wapate kusaidiwa!
*They have taken gods besides God, hoping that they might be helped.
|
36:75
لَا يَسْتَطِيعُونَ نَصْرَهُمْ وَهُمْ لَهُمْ جُنْدٌ مُحْضَرُونَ
*Hawataweza kuwasaidia. Bali hao ndio watakuwa askari wao watakao hudhurishwa.
*But they cannot help them, while they are an army mobilized for their defence.
|
36:76
فَلَا يَحْزُنْكَ قَوْلُهُمْ ۘ إِنَّا نَعْلَمُ مَا يُسِرُّونَ وَمَا يُعْلِنُونَ
*Basi maneno yao yasikuhuzunishe. Hakika Sisi tunayajua wanayo yaweka siri na wanayo yatangaza.
*So do not let their remarks grieve you. We indeed know whatever they hide and whatever they disclose.
|
36:77
أَوَلَمْ يَرَ الْإِنْسَانُ أَنَّا خَلَقْنَاهُ مِنْ نُطْفَةٍ فَإِذَا هُوَ خَصِيمٌ مُبِينٌ
*Kwani mwanaadamu haoni ya kwamba Sisi tumemuumba yeye kutokana na tone la manii? Kisha sasa yeye ndio amekuwa ndiye mgomvi wa dhaahiri!
*Does not man see that We created him from a drop of seminal fluid, and behold, he is an open contender!?
|
36:78
وَضَرَبَ لَنَا مَثَلًا وَنَسِيَ خَلْقَهُ ۖ قَالَ مَنْ يُحْيِي الْعِظَامَ وَهِيَ رَمِيمٌ
*Na akatupigia mfano, na akasahau kuumbwa kwake, akasema: Ni nani huyo atakaye ihuisha mifupa nayo imekwisha mung´unyika?
*He draws comparisons for Us, and forgets his own creation. He says, ‘Who will revive the bones when they have decayed?’
|
36:79
قُلْ يُحْيِيهَا الَّذِي أَنْشَأَهَا أَوَّلَ مَرَّةٍ ۖ وَهُوَ بِكُلِّ خَلْقٍ عَلِيمٌ
*Sema: Ataihuisha huyo huyo aliye iumba hapo mara ya mwanzo. Na Yeye ni Mjuzi wa kila kuumba.
*Say, ‘He will revive them who produced them the first time, and He has knowledge of all creation.
|
36:80
الَّذِي جَعَلَ لَكُمْ مِنَ الشَّجَرِ الْأَخْضَرِ نَارًا فَإِذَا أَنْتُمْ مِنْهُ تُوقِدُونَ
*Aliye kujaalieni kupata moto kutokana na mti wa kijani nanyi mkawa kwa huo mnawasha.
*—He, who made for you fire out of the green tree, and behold, you light fire from it!
|
36:81
أَوَلَيْسَ الَّذِي خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ بِقَادِرٍ عَلَىٰ أَنْ يَخْلُقَ مِثْلَهُمْ ۚ بَلَىٰ وَهُوَ الْخَلَّاقُ الْعَلِيمُ
*Kwani aliye ziumba mbingu na ardhi hawezi kuwaumba mfano wao? Kwani! Naye ndiye Muumbaji Mkuu, Mjuzi.
*Is not He who created the heavens and the earth able to create the like of them? Yes indeed! He is the All-creator, the All-knowing.
|
36:82
إِنَّمَا أَمْرُهُ إِذَا أَرَادَ شَيْئًا أَنْ يَقُولَ لَهُ كُنْ فَيَكُونُ
*Hakika amri yake anapo taka kitu ni kukiambia tu: Kuwa! Na kikawa.
*All His command, when He wills something, is to say to it ‘Be,’ and it is.
|
36:83
فَسُبْحَانَ الَّذِي بِيَدِهِ مَلَكُوتُ كُلِّ شَيْءٍ وَإِلَيْهِ تُرْجَعُونَ
*Basi Ametakasika yule ambaye mkononi mwake umo Ufalme wa kila kitu; na kwake Yeye mtarejeshwa.
*So immaculate is He in whose hand is the dominion of all things and to whom you shall be brought back.
|