بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ Kwa Jina La Mwenyezi Mungu, Mwingi Wa Rehema, Mwenye Kurehemu. |
52:1
وَالطُّورِ
*Naapa kwa mlima wa T´ur,
*By the Mount [Sinai],
|
52:2
وَكِتَابٍ مَسْطُورٍ
*Na Kitabu kilicho andikwa
*by the Book inscribed
|
52:3
فِي رَقٍّ مَنْشُورٍ
*Katika ngozi iliyo kunjuliwa,
*on an unrolled parchment,
|
52:4
وَالْبَيْتِ الْمَعْمُورِ
*Na kwa Nyumba iliyo jengwa,
*by the House greatly frequented,
|
52:5
وَالسَّقْفِ الْمَرْفُوعِ
*Na kwa dari iliyo nyanyuliwa,
*by the vault raised high,
|
52:6
وَالْبَحْرِ الْمَسْجُورِ
*Na kwa bahari iliyo jazwa,
*by the surging sea:
|
52:7
إِنَّ عَذَابَ رَبِّكَ لَوَاقِعٌ
*Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi hapana shaka itatokea.
*indeed your Lord’s punishment will surely befall.
|
52:8
مَا لَهُ مِنْ دَافِعٍ
*Hapana wa kuizuia.
*There is none who can avert it.
|
52:9
يَوْمَ تَمُورُ السَّمَاءُ مَوْرًا
*Siku zitakapo tikisika mbingu kwa mtikiso,
*On the day when the heaven whirls violently
|
52:10
وَتَسِيرُ الْجِبَالُ سَيْرًا
*Na milima iwe inakwenda kwa mwendo mkubwa.
*and the mountains move with an awful motion:
|
52:11
فَوَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِلْمُكَذِّبِينَ
*Basi ole wao siku hiyo hao wanao kadhibisha,
*woe to the deniers on that day
|
52:12
الَّذِينَ هُمْ فِي خَوْضٍ يَلْعَبُونَ
*Ambao wanacheza katika mambo ya upuuzi.
*—those who play around in vain talk,
|
52:13
يَوْمَ يُدَعُّونَ إِلَىٰ نَارِ جَهَنَّمَ دَعًّا
*Siku watapo sukumwa kwenye Moto kwa msukumo wa nguvu,
*the day when they will be shoved forcibly toward the fire of hell
|
52:14
هَٰذِهِ النَّارُ الَّتِي كُنْتُمْ بِهَا تُكَذِّبُونَ
*(Waambiwe): Huu ndio ule Moto mlio kuwa mkiukanusha!
*[and told:] ‘This is the Fire which you used to deny!’
|
52:15
أَفَسِحْرٌ هَٰذَا أَمْ أَنْتُمْ لَا تُبْصِرُونَ
*Je! Huu ni uchawi, au hamwoni tu?
*Is this, then, also magic, or is it you who do not perceive?
|
52:16
اصْلَوْهَا فَاصْبِرُوا أَوْ لَا تَصْبِرُوا سَوَاءٌ عَلَيْكُمْ ۖ إِنَّمَا تُجْزَوْنَ مَا كُنْتُمْ تَعْمَلُونَ
*Uingieni, mkistahamili au msistahamili - ni mamoja kwenu. Hakika mnalipwa kwa mliyo kuwa mkiyatenda.
*‘Enter it, and whether you are patient or impatient it will be the same for you. You are only being requited for what you used to do.’
|
52:17
إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي جَنَّاتٍ وَنَعِيمٍ
*Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na neema,
*The Godwary will indeed be amid gardens and bliss,
|
52:18
فَاكِهِينَ بِمَا آتَاهُمْ رَبُّهُمْ وَوَقَاهُمْ رَبُّهُمْ عَذَابَ الْجَحِيمِ
*Wakifurahi kwa yale aliyo wapa Mola wao Mlezi. Na Mola wao Mlezi atawalinda na adhabu ya Motoni.
*rejoicing because of what their Lord has given them and that their Lord has saved them from the punishment of hell.
|
52:19
كُلُوا وَاشْرَبُوا هَنِيئًا بِمَا كُنْتُمْ تَعْمَلُونَ
*Kuleni na kunyweni kwa raha kabisa kwa sababu ya mliyo kuwa mkiyatenda.
*[They will be told:] ‘Enjoy your food and drink as a reward for what you used to do.’
|
52:20
مُتَّكِئِينَ عَلَىٰ سُرُرٍ مَصْفُوفَةٍ ۖ وَزَوَّجْنَاهُمْ بِحُورٍ عِينٍ
*Watakuwa wameegemea juu ya viti vya enzi vilivyo pangwa kwa safu. Na tutawaoza mahuru-l-aini.
*They will be reclining on arrayed couches, and We will wed them to big-eyed houris.
|
52:21
وَالَّذِينَ آمَنُوا وَاتَّبَعَتْهُمْ ذُرِّيَّتُهُمْ بِإِيمَانٍ أَلْحَقْنَا بِهِمْ ذُرِّيَّتَهُمْ وَمَا أَلَتْنَاهُمْ مِنْ عَمَلِهِمْ مِنْ شَيْءٍ ۚ كُلُّ امْرِئٍ بِمَا كَسَبَ رَهِينٌ
*Na walio amini na dhuriya zao wakawafuata kwa Imani tutawakutanisha nao dhuriya zao, na wala hatutawapunja hata kidogo katika vitendo vyao. Kila mtu lazima atapata alicho kichuma.
*The faithful and their descendants who followed them in faith —We will make their descendants join them and We will not stint anything from their deeds. Every person is hostage to what he has earned.
|
52:22
وَأَمْدَدْنَاهُمْ بِفَاكِهَةٍ وَلَحْمٍ مِمَّا يَشْتَهُونَ
*Na tutawapa matunda, na nyama kama watavyo penda.
*We will provide them with fruits and meat, such as they desire.
|
52:23
يَتَنَازَعُونَ فِيهَا كَأْسًا لَا لَغْوٌ فِيهَا وَلَا تَأْثِيمٌ
*Watapeana humo bilauri zisio na vinywaji vya kuleta maneno ya upuuzi wala dhambi.
*There they will pass from hand to hand a cup wherein there will be neither any vain talk nor sinful speech.
|
52:24
وَيَطُوفُ عَلَيْهِمْ غِلْمَانٌ لَهُمْ كَأَنَّهُمْ لُؤْلُؤٌ مَكْنُونٌ
*Iwe wanawapitia watumishi wao kama kwamba ni lulu zilizomo katika chaza.
*They will be waited upon by their youths, as if they were guarded pearls.
|
52:25
وَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَاءَلُونَ
*Wataelekeana wakiulizana.
*They will turn to one another, questioning each other.
|
52:26
قَالُوا إِنَّا كُنَّا قَبْلُ فِي أَهْلِنَا مُشْفِقِينَ
*Waseme: Tulikuwa zamani pamoja na ahali zetu tukiogopa;
*They will say, ‘Indeed, formerly, we used to be apprehensive about our families.
|
52:27
فَمَنَّ اللَّهُ عَلَيْنَا وَوَقَانَا عَذَابَ السَّمُومِ
*Basi Mwenyezi Mungu akatufanyia hisani na akatulinda na adhabu ya upepo wa Moto.
*But God showed us favour and He saved us from the punishment of the [infernal] miasma.
|
52:28
إِنَّا كُنَّا مِنْ قَبْلُ نَدْعُوهُ ۖ إِنَّهُ هُوَ الْبَرُّ الرَّحِيمُ
*Hakika sisi zamani tulikuwa tukimwomba Yeye tu. Hakika Yeye ndiye Mwema Mwenye kurehemu.
*We used to supplicate Him in anticipation. Indeed, He is the All-benign, the All-merciful.’
|
52:29
فَذَكِّرْ فَمَا أَنْتَ بِنِعْمَتِ رَبِّكَ بِكَاهِنٍ وَلَا مَجْنُونٍ
*Basi kumbusha! Kwani wewe, kwa neema ya Mola wako Mlezi, si kuhani wala mwendawazimu.
*So admonish. By your Lord’s blessing, you are not a soothsayer, nor mad.
|
52:30
أَمْ يَقُولُونَ شَاعِرٌ نَتَرَبَّصُ بِهِ رَيْبَ الْمَنُونِ
*Au wanasema: Huyu ni mtunga mashairi, tunamtarajia kupatilizwa na dahari.
*Do they say, ‘He is a poet, for whom we await a fatal accident’?
|
52:31
قُلْ تَرَبَّصُوا فَإِنِّي مَعَكُمْ مِنَ الْمُتَرَبِّصِينَ
*Sema: Tarajieni, na mimi pia ni pamoja nanyi katika kutarajia.
*Say, ‘Wait! I too am waiting along with you.’
|
52:32
أَمْ تَأْمُرُهُمْ أَحْلَامُهُمْ بِهَٰذَا ۚ أَمْ هُمْ قَوْمٌ طَاغُونَ
*Au hizo akili zao ndio zinawaamrisha haya, au wao basi ni watu majeuri tu?
*Is it their intellects which prompt them to say this, or are they a rebellious lot?
|
52:33
أَمْ يَقُولُونَ تَقَوَّلَهُ ۚ بَلْ لَا يُؤْمِنُونَ
*Au ndio wanasema: Ameitunga hii! Bali basi tu hawaamini!
*Do they say, ‘He has improvised it himself?’ Rather they have no faith!
|
52:34
فَلْيَأْتُوا بِحَدِيثٍ مِثْلِهِ إِنْ كَانُوا صَادِقِينَ
*Basi nawalete masimulizi kama haya ikiwa wao wanasema kweli.
*Let them bring a discourse like it, if they are truthful.
|
52:35
أَمْ خُلِقُوا مِنْ غَيْرِ شَيْءٍ أَمْ هُمُ الْخَالِقُونَ
*Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji?
*Were they created from nothing? Or are they their own creators?
|
52:36
أَمْ خَلَقُوا السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ ۚ بَلْ لَا يُوقِنُونَ
*Au wao wameziumba mbingu na ardhi? Bali hawana na yakini.
*Did they create the heavens and the earth? Rather they have no certainty!
|
52:37
أَمْ عِنْدَهُمْ خَزَائِنُ رَبِّكَ أَمْ هُمُ الْمُصَيْطِرُونَ
*Au wanazo khazina za Mola wako Mlezi au wao ndio wenye madaraka?
*Do they possess the treasuries of your Lord? Or do they control them?
|
52:38
أَمْ لَهُمْ سُلَّمٌ يَسْتَمِعُونَ فِيهِ ۖ فَلْيَأْتِ مُسْتَمِعُهُمْ بِسُلْطَانٍ مُبِينٍ
*Au wanazo ngazi za kusikilizia? Basi huyo msikilizaji wao na alete hoja ilio wazi!
*Do they have a ladder [leading up to the heaven] whereby they eavesdrop? If so, let their eavesdropper produce a manifest authority.
|
52:39
أَمْ لَهُ الْبَنَاتُ وَلَكُمُ الْبَنُونَ
*Au Yeye Mwenyezi Mungu ana wasichana, na nyinyi ndio mna wavulana?
*Does He have daughters while you have sons?
|
52:40
أَمْ تَسْأَلُهُمْ أَجْرًا فَهُمْ مِنْ مَغْرَمٍ مُثْقَلُونَ
*Au wewe unawaomba ujira, na kwa hivyo ndio wanaelemewa na uzito wa gharama?
*Do you ask them for a reward, so that they are wary of being weighed down with debt?
|
52:41
أَمْ عِنْدَهُمُ الْغَيْبُ فَهُمْ يَكْتُبُونَ
*Au wanayo ilimu ya ghaibu, nao wameandika?
*Do they have access to the Unseen, which they write down?
|
52:42
أَمْ يُرِيدُونَ كَيْدًا ۖ فَالَّذِينَ كَفَرُوا هُمُ الْمَكِيدُونَ
*Au wanataka kufanya vitimbi tu? Lakini hao walio kufuru ndio watakao tegeka.
*Do they seek to outmaneuver God? But it is the faithless who are the outmaneuvered ones!
|
52:43
أَمْ لَهُمْ إِلَٰهٌ غَيْرُ اللَّهِ ۚ سُبْحَانَ اللَّهِ عَمَّا يُشْرِكُونَ
*Au wanae mungu asiye kuwa Mwenyezi Mungu? Subhanallah! Ametaksika Mwenyezi Mungu na hao wanao washirikisha naye.
*Do they have any god other than God? Clear is God of any partners that they ascribe to Him!
|
52:44
وَإِنْ يَرَوْا كِسْفًا مِنَ السَّمَاءِ سَاقِطًا يَقُولُوا سَحَابٌ مَرْكُومٌ
*Na hata wange ona pande linatoka mbinguni linaanguka wange sema: Ni mawingu yaliyo bebana.
*Were they to see a fragment falling from the sky, they would say, ‘A cumulous cloud.’
|
52:45
فَذَرْهُمْ حَتَّىٰ يُلَاقُوا يَوْمَهُمُ الَّذِي فِيهِ يُصْعَقُونَ
*Basi waache mpaka wakutane na siku yao watakapo hilikishwa.
*So leave them until they encounter the day when they will drop down dead;
|
52:46
يَوْمَ لَا يُغْنِي عَنْهُمْ كَيْدُهُمْ شَيْئًا وَلَا هُمْ يُنْصَرُونَ
*Siku ambayo hila zao hazitawafaa hata kidogo, wala wao hawatanusuriwa.
*the day when their guile will not avail them in any way, nor will they be helped.
|
52:47
وَإِنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُوا عَذَابًا دُونَ ذَٰلِكَ وَلَٰكِنَّ أَكْثَرَهُمْ لَا يَعْلَمُونَ
*Na hakika walio dhulumu watapata adhabu nyengine isiyo kuwa hii, lakini wengi wao hawajui.
*For those who do wrong, there is indeed a punishment besides that, but most of them do not know.
|
52:48
وَاصْبِرْ لِحُكْمِ رَبِّكَ فَإِنَّكَ بِأَعْيُنِنَا ۖ وَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ حِينَ تَقُومُ
*Na ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi. Kwani wewe hakika uko mbele ya macho yetu, na mtakase kwa kumsifu Mola wako Mlezi unapo simama,
*So submit patiently to the judgement of your Lord, for indeed you fare before Our eyes. And celebrate the praise of your Lord when you rise at dawn,
|
52:49
وَمِنَ اللَّيْلِ فَسَبِّحْهُ وَإِدْبَارَ النُّجُومِ
*Na usiku pia mtakase, na zinapo kuchwa nyota.
*and also glorify Him during the night and at the receding of the stars.
|