Sura 70 - Al-Ma'aarij

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
Kwa Jina La Mwenyezi Mungu, Mwingi Wa Rehema, Mwenye Kurehemu.

70:1
سَأَلَ سَائِلٌ بِعَذَابٍ وَاقِعٍ
*Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayo tokea,
*An asker asked for a punishment sure to befall
70:2
لِلْكَافِرِينَ لَيْسَ لَهُ دَافِعٌ
*Kwa makafiri - ambayo hapana awezaye kuizuia -
*—which none can avert from the faithless —
70:3
مِنَ اللَّهِ ذِي الْمَعَارِجِ
*Kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye mbingu za daraja.
*from Allah, Lord of the lofty stations.
70:4
تَعْرُجُ الْمَلَائِكَةُ وَالرُّوحُ إِلَيْهِ فِي يَوْمٍ كَانَ مِقْدَارُهُ خَمْسِينَ أَلْفَ سَنَةٍ
*Malaika na Roho hupanda kwendea kwake katika siku ambayo kadiri yake ni miaka khamsini elfu!
*The angels and the Spirit ascend to Him in a day whose span is fifty thousand years.
70:5
فَاصْبِرْ صَبْرًا جَمِيلًا
*Basi subiri kwa subira njema.
*So be patient, with a patience that is graceful.
70:6
إِنَّهُمْ يَرَوْنَهُ بَعِيدًا
*Hakika wao wanaiona iko mbali,
*Indeed they see it to be far off,
70:7
وَنَرَاهُ قَرِيبًا
*Na Sisi tunaiona iko karibu.
*and We see it to be near.
70:8
يَوْمَ تَكُونُ السَّمَاءُ كَالْمُهْلِ
*Siku ambayo mbingu zitakapo kuwa kama maadeni iliyo yayushwa.
*The day when the sky will be like molten copper,
70:9
وَتَكُونُ الْجِبَالُ كَالْعِهْنِ
*Na milima itakuwa kama sufi.
*and the mountains like [tufts of] dyed wool,
70:10
وَلَا يَسْأَلُ حَمِيمٌ حَمِيمًا
*Wala jamaa hatamuuliza jamaa yake.
*and no friend will inquire about [the welfare of his] friend,
70:11
يُبَصَّرُونَهُمْ ۚ يَوَدُّ الْمُجْرِمُ لَوْ يَفْتَدِي مِنْ عَذَابِ يَوْمِئِذٍ بِبَنِيهِ
*Ijapo kuwa wataonyeshwa waonane. Atatamani mkosefu lau ajikomboe na adhabu ya siku hiyo kwa kuwatoa fidia wanawe,
*[though] they will be placed within each other’s sight. The guilty one will wish he could ransom himself from the punishment of that day at the price of his children,
70:12
وَصَاحِبَتِهِ وَأَخِيهِ
*Na mkewe, na nduguye,
*his spouse and his brother,
70:13
وَفَصِيلَتِهِ الَّتِي تُؤْوِيهِ
*Na jamaa zake walio kuwa wakimkimu,
*his kin, which had sheltered him
70:14
وَمَنْ فِي الْأَرْضِ جَمِيعًا ثُمَّ يُنْجِيهِ
*Na wote waliomo duniani, kisha aokoke yeye.
*and all those who are upon the earth, if that might deliver him.
70:15
كَلَّا ۖ إِنَّهَا لَظَىٰ
*La, hasha! Kwa hakika huo ni Moto mkali kabisa,
*Never! Indeed, it is a blazing fire,
70:16
نَزَّاعَةً لِلشَّوَىٰ
*Unao babua ngozi ya kichwa!
*which strips away the scalp.
70:17
تَدْعُو مَنْ أَدْبَرَ وَتَوَلَّىٰ
*Utamwita kila aliye geuza mgongo na akageuka.
*It invites him, who has turned back [from the truth] and forsaken [it],
70:18
وَجَمَعَ فَأَوْعَىٰ
*Na akakusanya mali, kisha akayahifadhi.
*amassing [wealth] and hoarding [it].
70:19
إِنَّ الْإِنْسَانَ خُلِقَ هَلُوعًا
*Hakika mtu ameumbwa na papara.
*Indeed man has been created covetous:
70:20
إِذَا مَسَّهُ الشَّرُّ جَزُوعًا
*Inapo mgusa shari hupapatika.
*anxious when an ill befalls him
70:21
وَإِذَا مَسَّهُ الْخَيْرُ مَنُوعًا
*Na inapo mgusa kheri huizuilia.
*and grudging [charity] when good comes his way
70:22
إِلَّا الْمُصَلِّينَ
*Isipo kuwa wanao sali,
*—[all are such] except the prayerful,
70:23
الَّذِينَ هُمْ عَلَىٰ صَلَاتِهِمْ دَائِمُونَ
*Ambao wanadumisha Sala zao,
*those who persevere in their prayers
70:24
وَالَّذِينَ فِي أَمْوَالِهِمْ حَقٌّ مَعْلُومٌ
*Na ambao katika mali yao iko haki maalumu
*and there is a known share in whose wealth
70:25
لِلسَّائِلِ وَالْمَحْرُومِ
*Kwa mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba;
*for the beggar and the deprived,
70:26
وَالَّذِينَ يُصَدِّقُونَ بِيَوْمِ الدِّينِ
*Na ambao wanaisadiki Siku ya Malipo,
*and who affirm the Day of Retribution,
70:27
وَالَّذِينَ هُمْ مِنْ عَذَابِ رَبِّهِمْ مُشْفِقُونَ
*Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao Mlezi.
*and those who are apprehensive of the punishment of their Lord
70:28
إِنَّ عَذَابَ رَبِّهِمْ غَيْرُ مَأْمُونٍ
*Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuaminika nayo.
*(there is indeed no security from the punishment of their Lord)
70:29
وَالَّذِينَ هُمْ لِفُرُوجِهِمْ حَافِظُونَ
*Na ambao wanahifadhi tupu zao.
*and those who guard their private parts
70:30
إِلَّا عَلَىٰ أَزْوَاجِهِمْ أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُهُمْ فَإِنَّهُمْ غَيْرُ مَلُومِينَ
*Isipo kuwa kwa wake zao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi -
*(apart from their spouses and their slave women, for then they are not blameworthy;
70:31
فَمَنِ ابْتَغَىٰ وَرَاءَ ذَٰلِكَ فَأُولَٰئِكَ هُمُ الْعَادُونَ
*Lakini wanao taka kinyume ya haya, basi hao ndio wanao ruka mipaka.
*but whoever seeks beyond that—it is they who are the transgressors)
70:32
وَالَّذِينَ هُمْ لِأَمَانَاتِهِمْ وَعَهْدِهِمْ رَاعُونَ
*Na ambao wanazichunga amana zao na ahadi zao,
*and those who keep their trusts and covenants,
70:33
وَالَّذِينَ هُمْ بِشَهَادَاتِهِمْ قَائِمُونَ
*Na ambao wanasimama imara katika ushahidi wao,
*and those who are observant of their testimonies,
70:34
وَالَّذِينَ هُمْ عَلَىٰ صَلَاتِهِمْ يُحَافِظُونَ
*Na ambao wanazihifadhi Sala zao.
*and those who are watchful of their prayers.
70:35
أُولَٰئِكَ فِي جَنَّاتٍ مُكْرَمُونَ
*Hao ndio watakao hishimiwa Peponi.
*They will be in gardens, held in honour.
70:36
فَمَالِ الَّذِينَ كَفَرُوا قِبَلَكَ مُهْطِعِينَ
*Wana nini wale walio kufuru wanakutumbulia macho tu?
*What is the matter with the faithless that they scramble toward you,
70:37
عَنِ الْيَمِينِ وَعَنِ الشِّمَالِ عِزِينَ
*Makundi kwa makundi upande wa kulia na upande wa kushoto!
*from left and right, in groups?
70:38
أَيَطْمَعُ كُلُّ امْرِئٍ مِنْهُمْ أَنْ يُدْخَلَ جَنَّةَ نَعِيمٍ
*Kwani kila mmoja wao anatumai kuingizwa katika Pepo ya neema?
*Does each man among them hope to enter the garden of bliss?
70:39
كَلَّا ۖ إِنَّا خَلَقْنَاهُمْ مِمَّا يَعْلَمُونَ
*La, hasha! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na wanacho kijua.
*Never! Indeed, We created them from what they know.
70:40
فَلَا أُقْسِمُ بِرَبِّ الْمَشَارِقِ وَالْمَغَارِبِ إِنَّا لَقَادِرُونَ
*Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mashariki zote na magharibi zote kwamba Sisi tunaweza
*So I swear by the Lord of the easts and the wests that We are able
70:41
عَلَىٰ أَنْ نُبَدِّلَ خَيْرًا مِنْهُمْ وَمَا نَحْنُ بِمَسْبُوقِينَ
*Kuwabadili kwa walio bora kuliko wao; na Sisi hatushindwi.
*to replace them with [others] better than them and We are not to be outmaneuvered.
70:42
فَذَرْهُمْ يَخُوضُوا وَيَلْعَبُوا حَتَّىٰ يُلَاقُوا يَوْمَهُمُ الَّذِي يُوعَدُونَ
*Basi waache wapige porojo na wacheze, mpaka wakutane na siku yao wanayo ahidiwa,
*So leave them to gossip and play till they encounter the day they are promised:
70:43
يَوْمَ يَخْرُجُونَ مِنَ الْأَجْدَاثِ سِرَاعًا كَأَنَّهُمْ إِلَىٰ نُصُبٍ يُوفِضُونَ
*Siku watakapotoka makaburini kwa upesi kama kwamba wanakimbilia mfundo,
*the day when they emerge from graves, hastening, as if racing toward a target,
70:44
خَاشِعَةً أَبْصَارُهُمْ تَرْهَقُهُمْ ذِلَّةٌ ۚ ذَٰلِكَ الْيَوْمُ الَّذِي كَانُوا يُوعَدُونَ
*Macho yao yatainama, fedheha itawafunika. Hiyo ndiyo Siku waliyo kuwa wakiahidiwa.
*with a humbled look [in their eyes], overcast by abasement. That is the day they had been promised.